Filbert Msongela
143 posts













Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Dar es salaam Albert Msando, amesema Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Afrika Mashariki (KKAM) ambalo kwa wiki tatu limekuwa likitumiwa na Waumini wa KKAM na Waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la Askofu Josephat Gwajima kufanya Ibada, halijavunjwa kutokana na Waumini wa Gwajima kusali Kanisani hapo bali chanzo cha kuvunjwa kwake ni kutokana Kanisa hilo kujengwa ndani ya hifadhi ya barabara na tayari Uongozi wa Kanisa hilo ulishapewa notisi ya kuondoka eneo hilo. Akiongea na Mwandishi wa @AyoTV_, Bakari Chijumba wakiwa eneo lilipokuwa Kanisa hilo Ubungo Kibo Jijini Dar es salaam, DC Msando amesema Viongozi wa Kanisa hilo walishapewa notisi na TANROADS zaidi ya miezi miwili ya kutakiwa kuondoka eneo hilo na kusisitiza kuwa walipewa notisi hata kabla ya Waumini wa Gwajima kuanza kusali Kanisani hapo. Msando amesema Serikali haijawazuia Waumini wa Kanisa hilo kuendelea na Ibada na haiwezi kubomoa Kanisa kwasababu yao huku akisema hata leo Waumini hao wamefanya Ibada kwenye ukumbi wa Tanzanite Kimara Korogwe bila kuzuiwa na Polisi na amesema Jumapili ijayo yeye Msando atajumuika na Waumini wa Gwajima na watasali pamoja. Mwandishi alipotaka kujua kama DC Msando amewahi kuongea na Gwajima tangu kufungiwa kwa Makanisa yake na kama ikitokea akahudhuria Ibada Jumapili ijayo hatokamatwa, Msando amesema “Gwajima sijaongea nae hajawahi kunitafuta, akifika Kanisani kama atajielekeza kwenye yale ambayo yapo kwenye barua yake hatokamatwa na wala sio kwamba kutoonekana kwake ni kwasababu anakimbia Polisi kumkamata maana Polisi ikikuhitaji lazima itakupata” Video ya mahojiano Exclusive kati ya @AyoTV_ na DC Msando itapatikana katika chapisho linalofuata. #MillardAyoUPDATES






























