CyberKitz
1K posts






🚨𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄 Serikali ya Marekani imemzuia Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Jeshi la Polisi la Tanzania, Faustine Jackson Mafwele, kuingia nchini humo kutokana na madai ya kuhusika na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani (Department of State) imechukua hatua hiyo kufuatia taarifa zinazoaminika kuwa Mafwele alihusika katika ukiukwaji wa haki za binadamu. Mwaka mmoja uliopita, Jeshi la Polisi la Tanzania walidaiwa kuwakamata, kuwatesa, na kuwanyanyasa kingono raia wawili wa nchi jirani ambao ni Agather Atuhaire kutoka Uganda na Boniface Mwangi kutoka Kenya. Wawili hao walikuwa jijini Dar es Salaam kufuatilia mwenendo wa kesi ya kisheria ya kiongozi wa upinzani nchini Tanzania, Tundu Lissu. Marufuku hiyo imetangazwa na Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, chini ya Kifungu cha 7031(c) cha Sheria ya Bajeti ya Usalama wa Taifa, Wizara ya Mambo ya Nje, na Programu Zinazohusiana ya mwaka 2026. Sheria hii inazuia maafisa wa kigeni wanaohusika na ukiukwaji wa haki za binadamu kuingia Nchini Marekani. #MeaMswahiliUPDATES



Tiktok kuna masaibu jamani😹🙌






Federal Republic of The Great Lakes















Nimuuliza Mshabaha kwanini hakuniuliza, aliniambia kwamba walimuomba asiniambie. Nilimpigia simu Buyobe, nikamuuliza kwanin alimdanganya Mshabaha kwamba mimi ni Girlfriend wa Msuya wakati anajua mimi na Msuya hata hatufahamiani, alijiumauma sana mwisho akajitetea kwamba Msuya alimdanganya. Baada ya hapo ndo nilipost picha ya Msuya kuomba watu wanipe taarifa zake, na watu wengine pia wakapost. Taarifa zikaanza kutiririka ndo hapo tukajua kuwa Msuya baada ya kupiga tukio jioni ya siku hiyo hiyo, alionekana maeneo ya Namanga akivuka kuelekea Dar wakati huo Buyobe yeye alikimbilia maeneo ya Busia (Hii ni kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe) na hapo alifanya bila kuwasiliana na mtu yeyote hata wale waliompokea hakuwajulisha, licha ya kwamba awali wakati anafika alisema haijui kabisa Kenya ni mara yake ya kwanza kufika Kenya. Kupitia taarifa izo tulizopokea ndo tulijua kwamba Msuya na Buyobe ni marafiki tangu Buyobe akiwa anafanyakazi Tanroads na zamani walikuwa wakiishi majirani, maeneo ya Ubungo Msewe. Msuya baada ya kufika Dar alimpigia simu @ExMayorUbungo, akamuomba waonane maana anachafuliwa mitandaoni, Bony alikubalia so Msuya akaenda nyumban kwa Bony, alikiri kwamba ni kweli alienda Nairobi, ni kweli alionana na Mshabaha, Buyobe, Aziz na wale Wakenya wawili ila akasema hausiki na utekaji na wala hakuwepo kwenye tukio kabisa. Wakati Bony anazungumza na Msuya Buyobe alimpigia simu Msuya, akamwambia na yeye amekimbilia Busia maana ameona baada ya hilo tukio wale watoto watamng’ang’ania, wakapiga story kidogo then Buyobe akakata simu. Badae Bony alizungumza na Mshabaha ili asikilize na upande wake, Mshabaha akamueleze tukio lote akampa na ushaidi wa namna ambavyo Msuya amehusika. Bony alimpigia simu Msuya, akamuuliza wewe umesema haukuwepo eneo la tukio, mbona maeneo yote mlikopita unaonekana kwenye CCTV ukiwa pamoja nao, Msuya akamwambia ngoja kwanza nitakupigia ndo akapotea mazima. Baada ya kufeli kwa mpango wa kumteka Mshabaha na Wanaharaki wengine, Buyobe alirudi bongo licha ya kwamba alisema maisha yake yapo hatarini, Mafwele anamuwinda. Naomba niwarudishe nyuma kidogo baada ya Buyobe kuachiwa kwa dhamana alimpigia simu @IAMartin_ akamuelezea kwamba anaomba msaada wa Wakili kwasababu anatakiwa kwenda kuripoti Polisi. Aliunganishwa na Wakili then siku ya pili akasindikizwa kureport, wakati wanafika Chang’ombe Polisi njee ya kituo wakakutana na RCO, RPC, OCCID na Askari wengine ambao ni wapelelezi pamoja na Wanachama wa Chadema ambao na wao walikuwa wameenda kuripoti. Mashuhuda wanasema RCO alimuita Buyobe “Wewe njoo hapa” Buyobe akasogea walipo. RCO akamwambia chuchumaa chini, Buyobe akachuchumaa, RCO akamwambia, tumekupa dhamana kwanini umeenda mitandaoni kutushambulia kwa mambo ya uwongo au Tukufutie dhamana? Buyobe akaanza kujitetea kwamba account yake ya X (Twitter) inaendeshwa na watu wengi na aliyewashambulia kupitia account hiyo ni Martin Maranja Masese, RCO akachukua pen na karatasi akaandika jina la MM ili akamatwe na kuhojiwa, Halafu kipindi hiko ilikuwa ni baada ya Oktoba 29 watu walikuwa wanapewa kesi za uhaini sana. Wakili aliyemsindikiza pamoja na baadhi ya Wanachama wa Chadema waliokuwa pale njee wakamwambia Buyobe “Oya vipi mbona unataka kufanya mambo yawe makubwa, kwanini unataja watu ambao hawausiki” walimind sana. Badae Wakili alimshauri aombe msamaha, ndo Buyobe akaomba msamaha na Wakili nae akawa anakazia kwa kuwambia Polisi wamsamehe. Sasa wakati anaomba msamaha RCO na RPC wakaanza kumuuliza kwamba “Tuwaambie hawa watu wa Chadema ili wakujue wewe ni nan, unajifanya wewe ni mpambanaji/Mwanaharakati wewe ni Mwanaharakati kuanzia lini? Pale pale mbele ya wanachama wa Chadema na Wakili, Buyobe akaanza kuomba msamaha huku akimsihi RCO asitoboe siri “Nakuomba mkuu usiseme” RCO akawauliza watu wa Chadema kwamba nyie mnamtetea huyu jamaa mnajua vizuri? Watu wanasema kila mmoja alibaki anashangaa maana walikosa majibu wakati huo Buyobe yeye alikuwa amenywea, kimya!. Inaendelea part 4👇















