
Asia juma
108 posts








Mfungwa aliyehukumiwa jela miaka 30 kwa kesi ya ulawiti, Lista Chisoma, amemuomba Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kumuhurumia na kumpa msamaha wa kutoka gerezani wakati huu ambapo amebakiza miaka miwili ya kutumikia kifungo chake ambapo amemuomba Rais pia kuwa Wafungwa wengi wanahitaji huruma yake. Mfungwa amesema hayo leo May 09,2026 baada ya Rais Samia kufika kwenye banda ambalo halikuwa anashona wakati Rais akikagua mabanda kwenye shughuli ya kuhitimisha Mafunzo ya Uongozi Ngazi ya Juu Kozi Namba 28 na Uongozi Daraja la Pili Konzi Namba 48 kwa Mwaka 2025/2026 katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania. Mfungwa huyo amesema “Nimeingia nikiwa darasa la saba kwa msaada wa Megereza mwaka jana tumefanya mtihani wa form four utusaidie magereza kuna Watu wamekaa sana, mfano mie miaka 13 nimekaa, mtusaidie kuona jinsi gani tunasaidiwa, miaka miwili iliyobaki nisukumie nitoke nje, kule Magerezani kuna Watu wanahitaji huruma yako uwasaidie” #MillardAyoUPDATES







Haijawahi kutokea kwenye historia ya Ligi Kuu Bara Mchezaji kama Clatous Chota Chama, The Greatest ever.




















