Tanzania Political Index
6.7K posts

Tanzania Political Index
@IndexTanzania
Your go-to source for the latest political updates across Tanzania. | Tap to Join our WhatsApp Channel https://t.co/RwmKQjSJa0

Maria Sarungi ameamua kupambana na Buyobe kupitia parody yake ya @KatibaMpyaTz_ 😂😂😂. Maria hana tofauti na Godbless Lema na maparody yake ya Tanzania Abroad TV na Tanzania Leaks 🤡.






🚨 Msajili wa Vyama vya Siasa ameipa CHADEMA notisi ya kujieleza kuhusu tuhuma za kukiuka masharti ya Sheria ya Vyama vya Siasa katika shughuli zake. Kwa mujibu wa barua hiyo: 📌 CHADEMA inatuhumiwa kuendelea na mikutano na shughuli za chama chini ya kaulimbiu “No Reforms, No Election”, jambo ambalo Ofisi ya Msajili inaona linaweza kukiuka masharti ya usajili wa chama. 📌 Chama kimetakiwa kueleza kwanini kisichukuliwe hatua za kisheria, ikiwemo kusimamishwa usajili au kutozwa faini. 📌 Maelezo yanatakiwa kuwasilishwa kabla ya tarehe 20 Mei 2026 saa 6:00 mchana. Tunajua CHADEMA itaanza kampeni ya propaganda ya kudai inaonewa kwa sababu wao siku zote wanaona wako juu ya sheria. Sisi raia wema tunaomba Msajili wa Vyama vya Siasa afuate matakwa ya sheria hadi mwisho bila kupepesa macho ⚡

VITA YA GENGE LA WANAHARAKATI Jana tumeona "mwanaharakati" Mshabaha akimtupia tuhuma na shutuma nzito "mwanaharakati" mwenzie Buyobe aka paratropper. Mara nyingi ukiona hawa wanahaywa mitandaoni wakitupiana shutuma za usaliti na kuchomana ujue kuna mgongano wa maslahi. Yani wameingiliana kwenye ugali. Sasa ili mmoja aendelee kula ugali anatia mchanga ugali wa mwenzie. Ukweli uliogundulika ni kwamba kuna sehemu Buyobe alikua anaenda kupata fungu na hilo fungu hadi Maria na genge lake wamekua wakilifukuzia. Sasa ili Buyobe akose fungu hilo wapate wao ilikua lazima wamdiscredit kwenye jumuiya yao ya wanaharakati. Lakini kingine ni kwamba bwana Buyobe kuna siri ya kambi ya Maria anazifahamu na alikua anajiandaa kuziweka hadharani. Sasa ili wamuwahi na wao wajihami wakaamua kumtupia shutuma ili akija kusema siri zao umma usimuamini. Mimi nasema safi sana. Ukiwa kwenye meza ya wala nyama na nyama ikaisha lazima muanze kutafunana wenyewe kwa wenyewe. Tunasubiria sasa Buyobe amwagw mboga baada ya wakina Sarungi kumwaga ugali.


Tarehe 9 ya mwezi huu, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu (JWTZ), Meja Jenerali Fadhili Omar Nondo, alizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Bendera ya Taifa kwa washiriki wa Zoezi la 14 la Pamoja la Vituo vya Uamrishaji vya Kijeshi la Jumuiya ya Afrika Mashariki, linalofanyika nchini Kenya kuanzia leo tarehe 13 hadi tarehe 28 ya mwezi huu. Kwa hiyo taarifa ilishatoka mapema kabisa. Inawezekana ulikuwa bize na harakati za kupambania Katiba Mpya, ndiyo maana hili likakupita mdau…


It is time kuwa na public notice kuweni makini na @fbuyobe Jiepusheni naye kwa namna zote mnazoweza, vyovyote vile natumia hekima sana, Buyobe ana sura ya pili wengi msiyoijua, anachopost hapo na mambo anayofanya hapa Online sio anachoishi gizani Huyu sio mpambanaji

Tarehe 9 ya mwezi huu, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu (JWTZ), Meja Jenerali Fadhili Omar Nondo, alizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Bendera ya Taifa kwa washiriki wa Zoezi la 14 la Pamoja la Vituo vya Uamrishaji vya Kijeshi la Jumuiya ya Afrika Mashariki, linalofanyika nchini Kenya kuanzia leo tarehe 13 hadi tarehe 28 ya mwezi huu. Kwa hiyo taarifa ilishatoka mapema kabisa. Inawezekana ulikuwa bize na harakati za kupambania Katiba Mpya, ndiyo maana hili likakupita mdau…


JWTZ mko Kenya kuna shughuli gani mbona hakuna Tangazo la Joint Training au any official activity ? Hizi karibuni kumekuwa na maneno tata kutoka kwa Samia, JWTZ amkuona umuhimu kusema hii safari kuondoa hofu? Kuonyesha ni safari njema ?

KOCHA MZURI NI YULE ANAEJUA KUPANGA KIKOSI Kipimo cha kocha mzuri ni yule anaeweza kupangilia kikosi chake ikiwemo kusajili wachezaji, kupanga formation, kufanya substitution na vitu vingine vinavyoipa timu nafasi kubwa ya kufanikiwa. Kipimo cha ubora wa Rais ni namna anavyoteua watu katika nafasi mbalimbali kuhakikisha kwamba Serikali inatekeleza mipango yake kwa kiwango cha hali ya juu. Kwenye hili nimpongeze sana Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan. Nampongeza kwa sababu gani? Kwa sababu moja ya teuzi zake bora za kipindi chake hiki cha pili ni cha Waziri Mkuu Mwigulu Lameck Nchemba. Tumeshaona uwezo wake wa kusimamia shughuli za Serikali ndani ya nchi ila siku hizi mbili tumeshuhudia uwezo wake wa kuiwakilisha Taifa kwenye majukwaa ya kimataifa. Siku hizi mbili, Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba amemuwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa Ushirikiano wa Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya. Kwenye mkutano huo, Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba, amekutana na Rais wa International Fund for Agricultural Development (IFAD), Alvaro Lario, wakati Tanzania ikiharakisha ajenda yake ya mageuzi ya sekta ya kilimo. Tanzania inatarajia kutekeleza bajeti ya kilimo ya shilingi trilioni 1.1 kwa mwaka wa fedha 2026/27, ikiwa na lengo la kuongeza mchango wa sekta hiyo katika Pato la Taifa (GDP) hadi asilimia 36.3 ifikapo mwaka 2030, sambamba na mipango ya kufanya kilimo kuwa cha kibiashara na kuandaa kikamilifu ekari milioni 2.4 kwa miundombinu ya umwagiliaji. “Kimekuwa ni kikao kizuri kwa sababu tumekuwa na ushirikiano nao kwa muda mrefu, ambapo katika kipindi kilichopita tumeshirikiana nao katika miradi mbalimbali, na hasa miradi katika sekta za uzalishaji”.- Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba. Waziri Mkuu alishiriki pia chakula cha jioni cha kitaifa kilichoandaliwa na Rais wa Kenya Dkt. William Ruto kwa heshima ya Wakuu wa Nchi na Serikali wanaoshiriki Mkutano wa Ushirikiano wa Afrika na Ufaransa. Kwenye picha mbalimbali za hafla hiyo unaona kabisa jinsi Waziri Mkuu alivyo na muonekano wa statesman na jinsi ambavyo yuko nyumbani miongoni mwa viongozi wakuu wa bara la Afrika. Tunampongeza Rais Samia kwa uteuzi huu na tunampongeza Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba kwa kuendelea kuitendea haki nafasi aliyoaminiwa.














@Mwitah_tz Sina muda

Mtu umeomba Mkopo mwenyewe, Serikali wamekupa kila siku unaitisha press kutuelezea, Nondo bana 😂

