@MustapherM@MalisaGJ_ Maisha tu tamebadilika sana vyakula hali ya hewa nk lkn pia zaman pombe kali ilikuwa konyagi
Wanywaji wa gongo hao walikuwa wanaanguka wenyewe bila sababu nowadays ndio tumejua ni tatizo la figo
Kuna crisis kubwa sana ya Barabara Nchi hii…
Kuna ujambazi unafanyika kwenye aina ya ujenzi wanaofanya wachina! Barabara inajengwa nusu mwaka imeisha kabisa imekua kama mashimo ya ng’ombe..
Watu wanahongwa kuhujumu uchumi wa Nchi na kuhujumu wananchi.
Barabara ya Tarime - makutano imejengwa miaka ya 90’s bado ina uafadhali kuliko barabara ya Singida to Babati au Dodoma - Iringa za juzi tu..
Ukitoka Mwanza mpaka Bunda unaweza kulia, alafu eti kuna Waziri, makatibu wakuu, wakurugenzi, wakuu wa mikoa , Tanroads sijui na nani!!!
Utawala dhalimu umefitinika.
#TajiriLaKihaya
Twende mbele turudi nyuma…
Kama Mwanaume ukitulia ukatafakuri…
Utagundua kwamba hakuna Faida yoyote ya Kufanya mapenzi Nje ya Ndoa yako!
Ni akili tu Yakijinga…
UCHI HAUSHIBI…. hata ukipewa Mabinti wote duniani…. Bado utataka wa Mars … tena utataka hadi Aliens!
Kikubwa nkumuomba Mungu akupe Roho na moyo wa kuushinda Tamaa!
Alhamdulillah… mm usiku huu moyo huo na Roho hio NMEIPATA🙏🏽
Sasa hapa nijiandae tu Kuhiji Makkah Mwakani,In asha Allah!
Dhambi ya Uzinifu haitawahi nipata tena…
Am Born again!
“Much love, my friend—I miss you deeply. You are still one of the finest brains this country has. I’m keeping you in my prayers—may God give you the courage, strength, and resilience to rise above every challenge before you.”
@HildaNewton21 Hawa watu Lissu akiwafia magereza, hawatakuwa na jeshi la kuzuia hasira za Watanzania, na hawataweza kutembea hadharani maisha yao yote . Acha waendelee kucheza na hatari.
MHE LISSU AFIKISHWA MAHAKAMANI LEO
Leo Asubuhi, Mheshimiwa Lissu amefikishwa Mahakamani kusomewa uamuzi mdogo kufuatia Maombi yake ya kuunganishwa kwenye kesi ya Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya wadhamini wa Chama na Katibu Mkuu.
Kuna mambo mawili hapa ya kukumbuka; Mosi, Maombi ya Mhe Lissu yalisikilizwa na Mwanga hivyo kisheria yeye alipaswa kutoa uamuzi wa Maombi hayo.
Pili, Ikumbukwe kwamba jalada la kesi ya Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya wadhamini na Katibu Mkuu, lilishaondoka mezani kwake, lipo kwa Jaji Ngunyale.
Sasa, Jaji Mwanga katika uamuzi wake amekataa Maombi ya Lissu kuunganishwa kwenye hiyo kesi.
Ufafanuzi zaidi utatolewa na Chama.
Wakili @ShundoGaston ,
Mkurungenzi wa sheria wa CHADEMA HQ.
Ninaipongeza Klabu ya Simba kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Muungano mwaka 2026. Mbali na burudani, michezo imeendelea kuwa daraja imara linalotuunganisha.
Pia, ninazipongeza klabu zote nane zilizoshiriki mashindano hayo kwa kuonesha ushindani wa kirafiki na hamasa inayozidi kuimarisha tunu ya Muungano wetu.
‼️🚨BREAKING NEWS CHADEMA FREE TO CONTINUE POLITICAL ACTIVITIES - COURT RULES‼️
The Court of Appeal in Dodoma has ruled that the only real opposition party @ChademaTZ2 that was illegally banned from conducting political activities last year is now free to conduct activities as it wishes!
This is following IMMENSE pressure from international community, citizens and human rights activists! Much appreciation to all!
Yaani hapa wakubali wasikubali ukweli ni kuwa tuliwabana sasa wameachia mahakama ifuate sheria! Maana hadi Jaji Mkuu alikuwa analalamika kama sisi 😁 hizi “kelele” zetu za nje na ndani zimesaidia! Hongereni watanzania kwa kukataa kutishwa na kukaa kimya na asanteni mawakili! Kwa uongozi wa Chadema endeleeni kusimama kidete!
Sasa kimama akae kwa kutulia na amwachie Tundu Lissu maana kibano kiko palepale!
Nasema #TutaelewanaTu
George Sanga, msaliti wa Watanzania, amezua mjadala mpana katika jamii kufuatia hatua yake ya kubadili msimamo na kuacha njia ya mapambano ya haki na demokrasia. Kitendo chake kinatazamwa na wengi kama usaliti mkubwa dhidi ya jitihada za pamoja zilizojengwa kwa muda mrefu kwa gharama na mchango wa wananchi waliomuamini na kumsimamia katika nyakati ngumu.
Kwa mujibu wa kumbukumbu za matukio yaliyoshuhudiwa na umma, George Sanga aliwahi kukumbwa na kesi nzito ya mauaji iliyokuwa na adhabu kali. Katika kipindi hicho kigumu, Watanzania waliinuka kwa pamoja na kumuunga mkono kwa hali na mali, wakimchangia fedha za chakula akiwa gerezani, kusaidia familia yake kwa mahitaji ya kila siku, pamoja na kugharamia ada ya elimu ya mtoto wake. Baada ya kutoka gerezani, wananchi hao hao walimchangia mtaji ili aweze kurejea katika maisha ya kawaida.
Vilevile, viongozi na wanachama wa CHADEMA walionyesha mshikamano mkubwa kwa kufunga safari kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania kwenda kumtembelea na kumtia moyo alipokuwa kifungoni. Hatua hizi zilidhihirisha wazi imani na matumaini makubwa yaliyowekwa juu yake kama sehemu ya harakati za kuleta mabadiliko ya kweli nchini.
Hata hivyo, katika hali inayozua masikitiko makubwa, George Sanga ameondoka katika chama hicho na kujiunga na CHAUMA, huku akianza kutoa kauli za kejeli na dharau kwa wapigania haki na demokrasia. Aidha, hatua yake ya kuonekana kuwatetea wale waliowahi kumuweka gerezani imeibua hisia kali za kusalitiwa miongoni mwa wananchi waliowahi kusimama naye.
Mabadiliko haya ya ghafla ya msimamo yanaibua maswali makubwa kuhusu uaminifu, uadilifu na dhamira ya kweli ya viongozi ndani ya harakati za kijamii na kisiasa. Jamii inatarajia uwajibikaji na msimamo thabiti kutoka kwa wale wanaopewa dhamana ya kuongoza na kuwakilisha sauti za wananchi.
Wito unatolewa kwa wadau wote wa haki na demokrasia kuendelea kuwa imara, kushikamana na kutetea misingi ya haki na ukweli bila kuyumbishwa na matukio ya mtu mmoja. Mapambano ya haki na demokrasia hayawezi kusimamishwa na mabadiliko ya msimamo ya mtu binafsi, bali yataendelea kwa nguvu ya umma.
Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya kifo cha ndugu yetu, Mhe. William Lukuvi, ambaye nimepata heshima ya kufanya naye kazi kwa karibu ndani ya Bunge kwa kipindi cha miaka kumi, kuanzia mwaka 2010 hadi 2020.
Katika kipindi hicho chote, nimemfahamu kama kiongozi mzoefu, mahiri, na mwenye hekima kubwa katika utumishi wa umma. Alikuwa si tu mwakilishi wa wananchi, bali pia alikuwa sura ya Mkoa wa Iringa kwa muda mrefu—akisimama imara kulinda maslahi ya watu wake na taifa kwa ujumla.
Iringa leo imepoteza kiongozi shupavu na sauti muhimu ya maendeleo. Taifa kwa ujumla limepoteza mtumishi aliyekuwa na uzalendo wa dhati na moyo wa kujitoa.
Kwa niaba yangu binafsi, napenda kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, na wananchi wote wa Iringa. Tunamuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
Asante kwa utumishi wako, Mhe. Lukuvi. Tutakukumbuka daima.