𝘼𝙗𝙙𝙪𝙡
6.7K posts


Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, unatarajiwa kuagwa katika Mikoa Mitatu kabla ya kuzikwa Nyumbani kwake Idodi, katika Jimbo la Ismani Mkoani Iringa.
Kwa mujibu wa Ratiba ya Mazishi iliyotolewa, itaanza leo Machi 26, Jijini Dodoma ambapo Viongozi mbalimbali na Wananchi wataendelea kusaini Kitabu cha Maombolezo, huku mwili wa Kiongozi huyo ukitarajiwa kuwasili Nyumbani kwake majira ya jioni, na kisha tarehe 27, Machi kuagwa katika Viwanja vya Bunge ambapo Wabunge watapata nafasi ya kutoa Heshima ya mwisho kwa Kiongozi huyo.
Baadaye, Mwili huo utasafirishwa hadi Dar es Salaam kwa ajili ya kuagwa na Wananchi pamoja na Wadau mbalimbali katika Viwanja vya Karimjee, tarehe 28, Machi.
Ratiba hiyo itaendelea Mkoani Iringa kuanzia tarehe 29, Machi, ambako mwili wa marehemu utafikishwa kwa ajili ya kuagwa na Wananchi wa eneo hilo kabla ya kusafirishwa hadi Kijijini kwao Idodi kwa mazishi rasmi yatakayofanyika Machi 31, 2026.
Aidha, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Samia Suluhu Hassani anatarajiwa kuwaongoza Waombolezaji katika msiba huo.
Lukuvi, ambaye alikuwa Mbunge wa Isimani kwa muda mrefu, amefariki dunia Machi 25, 2026 Jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu. Kifo chake kimeacha pengo kubwa katika Uongozi na Siasa za Tanzania, huku akikumbukwa kwa mchango wake wa muda mrefu katika Utumishi wa umma.
#MillardAyoUPADATES.

Indonesia

@Royal_Tv_Tz Mmetumikia wananchi kwa miaka mingi acha wengine wafanye
Indonesia

Naibu Waziri wa Uchukuzi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mafinga Kusini mkoani Iringa, Mhe. David Kihenzile, amesema Serikali imepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu).
Akizungumza kufuatia kifo hicho, Mhe. Kihenzile alieleza kuwa marehemu atakumbukwa kwa uzalendo wake wa hali ya juu, uchapakazi, uaminifu pamoja na utiifu wake kwa Serikali, hasa katika kuisimamia na kuitetea kwa hoja zenye mashiko.
Indonesia
𝘼𝙗𝙙𝙪𝙡 retweetledi

Unaambiwa hata kitambaa cheupe ni yake .....
EL SUKAYO FIELD MARSHAL🇹🇿@Elsukay0
Kumbe Tin white ndo mmiliki halali wa Aslay mihogo?
हिन्दी

Jeshi la Magereza nchini Tanzania limetoa kanusho kali dhidi ya taarifa zilizochapishwa na baadhi ya magazeti leo, zikidai kuwa hali ya afya ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ni mbaya na inatia shaka.
Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo, Jumatano, Machi 25, 2026, jijini Dodoma, Msemaji wa Jeshi la Magereza, SACP Elizabeth G. Mbezi, amesisitiza kuwa taarifa hizo siyo sahihi na zimelenga kuleta taharuki isiyo na msingi katika jamii.
“Kimsingi taarifa hiyo siyo sahihi ni ya kuupuzwa kwani ina lengo la kuleta taharuki katika jamii. Jeshi linapenda kuujulisha umma kuwa ndugu Tundu Lissu yuko salama na afya yake ni njema”, imeeleza taarifa hiyo
SACP Mbezi ametoa wito kwa waandishi wa habari nchini kufuata misingi ya taaluma yao, ikiwemo kuhakiki taarifa kutoka kwenye vyanzo sahihi kabla ya kuzisambaza kwa umma. Amesema Jeshi hilo linatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria, kanuni, na taratibu huku likithamini utu na haki za binadamu kwa wafungwa na mahabusu wote.
Taarifa hii inakuja siku kadhaa baada Lissu kuieleza Mahakama ya Rufani yuko katika hatari ya afya yake kuathirika zaidi kwa kushindwa kuhudhuria kliniki ya matibabu yake kutokana na kushikiliwa mahabusu kwa muda mrefu.
Aliiomba Mahakama hiyo kulisikiliza kwa dharura shauri la mapitio lililofunguliwa mahakamani hapo na Jamhuri dhidi yake kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu, kuikatalia kuwasilisha ushahidi mpya katika kesi ya uhaini inayomkabili, ambalo limesababisha usikilizwaji wa kesi hiyo kusimama kwa muda usiojulikana.
Alidai kama shauri hilo lisiposikilizwa na kuamuliwa haraka basi hali ya afya yake itazidi kuathirika kwa kuzidi kukosa huduma hizo za kiafya kutokana na kuendelea kushikiliwa mahabusu, hivyo kupata madhara ambayo hayataweza kurekebishika na kukwamisha haki kutendeka.
Lissu alielezea hofu yake hiyo ya kuathirika kwa kukosa huduma za kiafya wakati alipowasilisha majibu yake ya maandishi dhidi ya hoja za Jamhuri katika shauri hilo la mapitio.

Indonesia

Wauaji mmeona inavouma eeeh?????
Sasa afadhali nyie familia yake mnalia huku mnauhakika mwili wa Lukuvi upo Mochwari.
Sasa fikirieni wenzenu ndugu zetu waliuwawa Oktoba 29 kwa risasi halafu Serikali ikaiba maelefu ya miili ya wapendwa wetu na kwenda kuizika kama mizogo kwenye makaburi ya Halaiki.
Halafu tukiwa katikati ya maumivu makali ambayo hayaelezeki tunamskia Baba yenu Lukuvi anaongea Bungeni kwamba Oktoba 29 amani na utulivu vilitamalaki,
Yani wameuwa ndugu zetu na bado wakawa wanaongea lugha za kejeli bila kujali tulikuwa na maumivu kiasi gani ndani ya mioyo yetu.😭
Kuna time nilikuwa najiuliza maswali mengi kuna muda nikadhan kwamba labda wao wataishi milele kumbe na wao huwa wanakufa.
Yani wanatuuwa kwa risasi, kututeka na kutupoteza halafu mwisho wa siku na wao wanakufa.
Huu Uchungu aliona Mke wa Lukuvi leo ndo huu huu anao Mke wa Mdude, ndo huu huu anapitia Mama wa Polepole, ndo huu huu wanapitia maelefu ya Wamama wa Watanganyika ambao wanaume zao na Vijana wao waliuliwa Oktoba 29.
Wapendwa tenda wema maana wema utakufuata hadi kaburini kwako.
Ukitenda mabaya, mabaya yako yatakufuata mpaka kaburini kwako.
Indonesia

@RevocatusMagum1 ww nae ukiona mtu kauliza na ww unajifanya kuuliza pungavu mkubwa
Indonesia

Ila “JOISI WOWOWO”.
Hawa ndio waliwaahidi kuwapa KATIBA MPYA na wakasema ndio kipaombele chao sio?
Saizi wanayo mipango ya kutawala tena 2030 na sio kutimiza ahadi walizowapa 2025. Hawa watu wapo tayari kuuwa kila mtu atakae onakana kikwazo kwao kutawala watanzania.
Jitu kama hili lenye uliki mzito kama MAVI YA TEMBO unafikiri linatuwazia nini sisi tunaowakosoa zaidi ya KUTEKA NA KUUWA?
Yapo duniani kuhakikisha yanatawala mpaka yanakufa na yanaona kama nchi hii ni ya wazazi wao sisi wengine wageni.
TUTAKUWEPO🫵🏾😎

Filipino

@TruthWatchDogTZ kwa hiyo depay nae?? yaani kwa mfano angechora nini pale yanga??
Indonesia

@fintanjr_ kibabage yupo sahihi tu coz kuna wachezaji wa yanga wanaipenda yanga lkn hawana icon ya kuichora kuashilia mapenzi ya timu yao
Indonesia

Nimeona wadau wakiwa na maoni tofauti tofauti kuhusu tatoo ya Kibabage, akiwa amechora tatoo ya Simba, lakini hajasema simba yule anamaanisha nini kwenye maisha yake, hii picha huyu ni Memphis Depay , haijui hata Simba SC ila ana hii tatoo,.. So Kibabage ametembea na upepo ila maana ya tatoo anaijua yeye,..
nb. Mtu akitaka kuchora Chura budget kwangu😂🐸🚮.

Filipino

TANZIA
Aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Lukuvi amefariki dunia katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Taarifa ya kifo chake imetangazwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Indonesia

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kifo cha Mbunge wa Jimbo la Isimani na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), William Vangimembe Lukuvi, kilichotokea leo tarehe 25 Machi, 2026, majira ya saa moja asubuhi katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa Moyo.
Taarifa hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na kusainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Moses Kusiluka.
Marehemu Lukuvi alikuwa akihudumu kama Mbunge wa Isimani Mkoani Iringa na Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu wa shughuli za Serikali, pamoja na masuala ya watu wenye Ulemavu.
Rais Samia ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Familia ya marehemu, Ndugu, Jamaa, Wananchi wa Jimbo la Isimani na Watanzania wote kwa ujumla.
#MillardAyoUPDATES

Indonesia

















