HamisZmc
3.4K posts


@sonnino123 Yule jamaa binafsi sina cha kumpa Mungu tu ampe Maisha marefu yenye afya na mafanikio tele.
Indonesia


@hamisZmc Niko njema sana, sema tu leo nimeamka na ka uchovu, ninejipa likizo ya wiki moja

@Fungothe2Nd @godbless_lema Sio kila sehemu alipo daktari mtaalam wa lishe atakuwepo... Daktari atafanya kazi yake kwa mgonjwa katika elimu ya lishe na mtaalamu wa lishe pia ana jukumu lake kwa mgonjwa
Indonesia

Afya ya binadamu ina uhusiano wa moja kwa moja na chakula anachokula. Pamoja na hilo, mfumo wa afya duniani umejikita zaidi kwenye tiba ya magonjwa kwa kutumia dawa badala ya kuzuia magonjwa kupitia lishe sahihi. Hali hii imechangia kuongezeka kwa magonjwa sugu kama kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo.
Lishe ni msingi wa afya ya mwili. Mwili hujijenga, hujirekebisha na kujilinda dhidi ya magonjwa kwa kutumia virutubisho vinavyopatikana kwenye chakula. Daktari asiye na uelewa wa kina kuhusu lishe humtibu mgonjwa kwa dawa bila kushughulikia chanzo halisi cha tatizo.
Kuwajengea madaktari elimu ya lishe kutasaidia kuzuia magonjwa kabla hayajatokea, kupunguza utegemezi wa dawa, na kuboresha maisha ya wagonjwa kwa muda mrefu. Aidha, gharama za huduma za afya zingepungua kwa kiasi kikubwa iwapo kinga ingekuwa kipaumbele kuliko tiba.
Kwa hiyo, elimu ya lishe kwa madaktari si hiari bali ni hitaji la msingi. Daktari anayeelewa lishe hutibu mwili mzima, si dalili pekee, na hilo ndilo lengo halisi la tiba.
Kwa hiyo, Tanzania pia inapaswa kufikiria kwa kina kujumuisha elimu ya lishe kama sehemu ya msingi katika mafunzo ya udaktari. Hatua hii itasaidia kujenga taifa lenye afya bora, tija kazini na maendeleo endelevu.

Indonesia

@godbless_lema Tanzania bado wataalamu wa Lishe hawajapewa kipaumbele katika kufanya kazi yao, kwanza wametengwa na mfumo mzima wa Afya, hawachukuliwi kama sehemu ya kada ya afya. Na hata majukumu wanayopangiwa unaona kabisa hayawapi nafasi ya kutumia walichokisoma kusaidia jamii.
Indonesia

Unalipenda kanisa au umempenda huyu mtawa ndugu muumini?
Hamadi.Mbeyale🔥🔥@hamadimbeyale
Nimejikuta nalipenda tu kanisa la Roman Cathoric: Wewe je ?.
Indonesia

Pumzika kwa amani, my dear uncle. Utaendelea kuishi mioyoni mwetu milele.
Utakumbukwa kwa mengi sana, Uncle. Taifa litakukumbuka kwa utumishi wako wa kihistoria kama Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania, ambapo ulisimamia kuanzishwa kwa sarafu ya Tanzania - Shillingi na kuweka misingi ya benki kuu ya taifa baada ya uhuru. Pia, katika wadhifa wako kama Waziri wa Fedha na Mipango, ulichangia kwa kiasi kikubwa katika sera za kiuchumi za taifa. Mimi binafsi, nitakukumbuka zaidi kwa juhudi zako za kugombea ubunge kupitia tiketi ya CCM, safari iliyojaa matumaini lakini pia mafunzo makubwa ya maisha.
Nakumbuka mwaka 1990, ulipokuja Makao Makuu ya Ushirika (CUT), Mtaa wa Lumumba, Jijini Dar es Salaam, nami nikiwa Afisa Uhusiano, CUT. Tulikutana gorofa ya 8, ukiwa umefika kurejesha fomu ya kugombea Ubunge kupitia viti sita vya Jumuiya ya Ushirika. Ilikuwa safari iliyojaa matumaini makubwa, lakini jina lako likakatwa katika mchakato wa ndani wa CUT, yakabaki majina ya Mwenyekiti wa CUT Phillipo Ndaki na Katibu Mkuu David Hollela.
Idadi ya wagombea ilipunguzwa makusudi ili kupunguza ushindani, kwani katika kipindi cha chama kimoja, Jumuiya za Ushirika, Vijana, Wanawake, Wazazi na Wafanyakazi zilikuwa zinapewa nafasi sita kila moja ya kupendekeza wagombea wa Ubunge, ambao baadaye walipigiwa kura na wabunge wa majimbo. Kati ya jumla ya wagombea 30, Bunge lilikuwa linachagua 15 tu. Ushirika, badala ya kupeleka majina 6, ilipeleka mawili tu, na kati ya hao, Mzee Phillipo Ndaki ndiye aliyechaguliwa. Hatimaye, Ushirika ukapata kiti kimoja tu.
Wanaushirika, hususan wakulima, walisikitika sana. Minong’ono ilikuwa mingi; maumivu, maswali, na kukata tamaa vilitawala. Hata hivyo, maisha yana njia zake za kutufundisha, hata pale tunapohisi tumenyimwa haki.
Mwaka 1992 vyama vingi vya siasa viliporuhusiwa, ulisimama tena kwa ujasiri. Safari mpya ikaanza, ukiwa mmoja wa waasisi wa CHADEMA na Mwenyekiti wake wa kwanza. Leo, tunapotafakari kwa kina, tunaona wazi kuwa kile kilichoonekana kama kushindwa kilikuwa maandalizi ya kusudi kubwa zaidi. Huenda kama jina lako lingepitishwa kugombea ubunge kupitia CCM, viti maalum vya Jumuiya ya Ushirika, CHADEMA ingechelewa au isingezaliwa kwa wakati wake.
Hilo ndilo funzo kubwa kwetu sote:
Kukataliwa leo si mwisho wa safari; mara nyingi ni mlango wa wito mkubwa zaidi kesho.
“Nimepiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, imani nimeilinda.”
— 2 Timotheo 4:7
Umeacha historia, funzo, na urithi usiofutika.
Lala salama, Uncle. Umetutoka tarehe 19/01, siku yenye kumbukumbu nzito katika familia yetu, siku ya kuzaliwa marehemu mjomba wako na shemeji yako, baba yangu, Mzee Gaspar Marealle, aliyetwaliwa tarehe 16 Mei 2024 akiwa na miaka 103!




Indonesia

Wadogo zangu Mwenyezi Mungu amenipa kibali ..Nilikuwa nawaomba mkanipigie kura ikiwapendeza🙏
🇪 🇸 🇮 🇷 🇹🇿🇲 🇹 🇿@EsirEid
#TajiriLaKihaya Kati ya FEMALES Walio Comment na Ku QUOTE Hawa wawili @Tinahcristiaan na @ShirimaYvonne wamekidhi vigezo tulivyovitaja na kuvihitaji. Ila tunahitaji mtu mmoja tu atakaechukua 500k. PIGA KURA HAPO KWENYE COMMENT kabla ya saa sita usiku huu!
Indonesia















