Ntele B H retweetledi

ZIARA YA MWENYEKITI WA KANDA YA PWANI KATIKA JIMBO LA MBAGALA,
Jana tarehe 3 Mei 2026, Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani Mhe. @ExMayorUbungo, akiambatana na viongozi mbalimbali wa ngazi ya Kanda na Mkoa wa Temeke, amefanya ziara ya kikazi katika Jimbo la Mbagala.
Uwekaji wa Jiwe la Msingi: Mwenyekiti ameweka jiwe la msingi katika jengo la Ofisi ya Chama Jimbo la Mbagala. Jengo hilo hivi sasa lipo katika hatua za ujenzi, likiwa ni sehemu ya mpango wa kuimarisha miundombinu ya Chama.
Ufunguzi wa Misingi: Aidha, Mwenyekiti amefungua rasmi msingi wa Chama katika Tawi la Mikwambe, lililopo Kata ya Toangoma. Hatua hii inalenga kuimarisha uhai wa Chama kuanzia ngazi ya chini kabisa.
Ziara hii ni sehemu ya mkakati endelevu wa Kanda ya Pwani kuhakikisha kuwa kila jimbo linakuwa na ofisi bora na ya kisasa. Uwepo wa ofisi hizi utasaidia:
1.Kuboresha mazingira ya kupanga mikakati ya ushindi.
2.Kutoa nafasi rasmi na tulivu kwa ajili ya kutekeleza shughuli za kila siku za Chama.
Chama Imara, Ofisi Bora kwa Maendeleo ya Jimbo.




Indonesia























