
JogooFarm
1.4K posts

JogooFarm
@ufugaji58com
Mfugaji, mjasiliamali. Kuku for life. Local chicken, kuroiler, broiler, Tujiahiri, tufuge pamoja.




































👉Kuna muhimu mkubwa kufanyika kwa uchunguzi wa dharura kwa kuundwa kwa tume huru itakayochunguza kwa kina mwenendo wa sekta ya mafuta nchini, kwa lengo la kulinda maslahi mapana ya taifa na kuhakikisha uwazi katika maamuzi yanayogusa uchumi wa wananchi. 👉Taasisi za umma zinazohusika moja kwa moja na mafuta kama TPDC, PBPA, EWURA, TPA pamoja na Wizara ya Nishati zina wajibu mkubwa wa kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unakuwa wa uhakika na kwa gharama nafuu kwa wananchi wote. 👉Endapo kutakuwa na dosari, ucheleweshaji au maamuzi yenye kuashiria mgongano wa maslahi binafsi ndani ya taasisi hizi, ni lazima hatua zichukuliwe mapema ili kuzuia madhara makubwa kwa uchumi wa nchi. 👉Wananchi wanahitaji maelezo ya wazi kuhusu sababu za kupanda kwa bei ya mafuta mapema kuliko ilivyotarajiwa, hasa baada ya taarifa ya Machi 23, 2026 kueleza kuwa akiba ya mafuta ingekuwa ya kutosha hadi Julai 2026. 👉Tofauti ya muda kati ya matarajio yaliyotolewa na hali halisi ya kupanda kwa bei inaleta maswali mengi kuhusu uwazi wa taarifa na uhalali wa maamuzi yaliyofanyika ndani ya mfumo wa usimamizi wa mafuta. 👉Kunatakiwa Kuwe na muhimu kuchunguza kama kuna uwezekano wa uwepo wa mianya inayoweza kuruhusu baadhi ya watendaji kunufaika binafsi kupitia biashara ya mafuta, hali ambayo inaweza kuathiri ustawi wa wananchi wengi. 👉Sekta ya mafuta ina athari kubwa kwa gharama za maisha, kwani kupanda kwa bei ya mafuta husababisha kuongezeka kwa gharama za usafirishaji, uzalishaji na hatimaye kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali. 👉Tume huru itasaidia kurejesha imani ya wananchi kwa kuhakikisha kuwa taratibu zote zinazohusiana na ununuzi, usambazaji na upangaji wa bei ya mafuta zinafuata sheria na misingi ya uwajibikaji. 👉Uwazi na uwajibikaji ni nguzo muhimu katika kulinda uchumi wa taifa, hivyo ni vyema mamlaka husika zikatoa ufafanuzi wa kina ili kuondoa sintofahamu iliyopo miongoni mwa wananchi. 👉Kwa maslahi mapana ya taifa, uchunguzi wa haraka na wa haki utasaidia kubaini ukweli, kuchukua hatua stahiki na kuhakikisha sekta ya nishati inawanufaisha wananchi wote badala ya wachache✍️



Naanza kuamini kwamba kuna wanawake wanadawa za kuwashika wanaume wao. Kuna mwanangu mmoja amepambana na mkewake katika kuugua. Mwanamke anaumwa mara kwa mara, baada ya muda akapima HIV akakuta positive. Msela akamuachia geto na watoto, ila now wanakaa pamoja tena. MADAWA.












